Saturday 13 September 2014

Diamond kuchuana tena na Davido kwenye tuzo za MTVEMA

Msimu wa tuzo za MTV Europe MTVEMA uko mbioni na tayari majina manne ya wasanii watakaowania tuzo hizo yameshatolea, Diamond Platnumz akiwa ni mmoja wapo


Diamond atakuwa akichuwana kwa mara nyingine tena na msanii kutoka Nigeria Davido, Goldfish
(south Africa) pamoja na Toofan (Togo)
EMA wametoa nafasi na kuwapa nguvu mashabiki na wapenda mziki wote duniani kumchagua mshiriki atakaekuwa wa tano katika kipengele hicho (Best African Act) kupitia mitandao ya kijamii wakimchagua kutoka katika list hii ya wasanii


Anselmo Ralph - #NominateAnselmoRalph
Gangs of Ballet - #NominateGangsOfBallet
Mafikizolo - #NominateMafikizolo
Sarkodie - #NominateSarkodie
Sauti Sol - #NominateSautiSol
Tiwa Savage - #NominateTiwaSavage

upigaji kura umeshaanza na uko wazi mpaka tarehe 14 September 2014 @ 11:59 CAT.  Majina yote ya watakaokuwa wakiwania tuzo hizo yatatangazwa  na upigaji kura utakuwa wazi kuanzia  16 September 2014.

Tuzo hizo za  MTV EMA” zitarushwa live na MTV Channel 130 jumapili 9 November  22:00 CAT kutooka Glasgow, Scotland

No comments:

Post a Comment