The Last Breath - 1
Mwaa!” Loveness alimbusu Johnson
kwenye paji la uso, kisha akageukia upande wa pili na kumbusu shavuni mtoto wao
Melania, binti yao mwenye umri wa miaka mitatu!
Moyoni mwake alisikia uchungu mno, hakuna kitu alichokichukia kama kuagana na watu aliowapenda. Kwa hakika mume wake Johnson na binti yake Melania, ndiyo walikuwa watu pekee aliowapenda kuliko wengine wote chini ya jua la Mungu.
Moyoni mwake alisikia uchungu mno, hakuna kitu alichokichukia kama kuagana na watu aliowapenda. Kwa hakika mume wake Johnson na binti yake Melania, ndiyo walikuwa watu pekee aliowapenda kuliko wengine wote chini ya jua la Mungu.
Kwa nguvu zake zote alijitahidi
kuyazuia machozi yasimlengelenge lakini haikuwezekana, taratibu yakazipenya
kope na kuanza kushuka kuelekea mashavuni, Johnson akachukua kitambaa mfukoni
kwake na kuanza kumfuta huku akimtuliza asiendelee kulia mbele ya mtoto.
“Mpenzi si utakuja nyumbani kwenye Sikukuu ya Krismasi?”
“Ndiyo.”
“Kuanzia sasa mpaka Krismasi bado
siku ngapi?”
“Kama mwezi mmoja hivi.”
“Sasa kwa nini unalia?”
“Sijielewi, moyoni mwangu nahisi kama nawaona kwa mara ya mwisho!” Loveness aliongea na kuzidi kububujikwa na machozi.
“Kama mwezi mmoja hivi.”
“Sasa kwa nini unalia?”
“Sijielewi, moyoni mwangu nahisi kama nawaona kwa mara ya mwisho!” Loveness aliongea na kuzidi kububujikwa na machozi.
“Mama acha kulia!” Melania
alimwambia mama yake na kumfanya ajisikie vibaya.
Katika maisha yake yote tangu azaliwe, Loveness alishasindikiza watu wengi sana stendi za basi, viwanja vya ndege, bandarini waliokuwa wakiondoka na kumwacha, ni kweli aliumia na kusikitika na ndiyo maana alizichukia sana sehemu hizo, lakini siku hiyo aliumia zaidi kuliko siku nyingine zilizotangulia, kuna sauti ilimwambia kutoka ndani kabisa kwamba asingewaona tena lakini alibishana nayo.
“Kwa kweli ungekuwa uwezo wangu, ningewazuia msisafiri!”
“Kwa nini?”
Katika maisha yake yote tangu azaliwe, Loveness alishasindikiza watu wengi sana stendi za basi, viwanja vya ndege, bandarini waliokuwa wakiondoka na kumwacha, ni kweli aliumia na kusikitika na ndiyo maana alizichukia sana sehemu hizo, lakini siku hiyo aliumia zaidi kuliko siku nyingine zilizotangulia, kuna sauti ilimwambia kutoka ndani kabisa kwamba asingewaona tena lakini alibishana nayo.
“Kwa kweli ungekuwa uwezo wangu, ningewazuia msisafiri!”
“Kwa nini?”
“Najisikia vibaya mno Johnson,
nahisi kuna tatizo litatokea!”
“Hapana, hizo ni hisia tu mpenzi! Acha nimrudishe Melania Dar es Salaam, Jumatatu anatakiwa darasani, si unajua likizo yenyewe ilikuwa ni ya wiki moja tu, tumekuona mpenzi, utatukuta Dar es Salaam utakapokuja na safari hii ninataka nikufanyie ‘sapraizi’ ambayo hutaisahau maishani mwako!”
“Sapraizi gani?”
“Hapana, hizo ni hisia tu mpenzi! Acha nimrudishe Melania Dar es Salaam, Jumatatu anatakiwa darasani, si unajua likizo yenyewe ilikuwa ni ya wiki moja tu, tumekuona mpenzi, utatukuta Dar es Salaam utakapokuja na safari hii ninataka nikufanyie ‘sapraizi’ ambayo hutaisahau maishani mwako!”
“Sapraizi gani?”
“Wewe utaona ukija, siwezi kukuambia
sasa hivi!” Johnson aliongea, ingawa moyoni mwake alielewa alitaka kumnunulia
mke wake gari mpya aina ya Range Rover Evoque.
Zamu yao ya kuingia uwanjani ikafika, hawakuwa na namna tena ya kuendelea kubaki nje, muda wa kuiacha Kinshansa ulikuwa umefika na pia kumwacha Loveness peke yake akiendelea na kazi katika Shirika la Kimataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR) ambalo ofisi zake zilikuwepo katika jiji hilo, alikofanya kazi kama Afisa Ustawi wa Jamii.
Zamu yao ya kuingia uwanjani ikafika, hawakuwa na namna tena ya kuendelea kubaki nje, muda wa kuiacha Kinshansa ulikuwa umefika na pia kumwacha Loveness peke yake akiendelea na kazi katika Shirika la Kimataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR) ambalo ofisi zake zilikuwepo katika jiji hilo, alikofanya kazi kama Afisa Ustawi wa Jamii.
Loveness alimwangalia Johnson
machoni, akahamishia tena kwa mtoto wake, akakosa nguvu za kuwaangalia,
akainamisha uso wake chini, machozi yakadondoka sakafuni! Alichokifanya Johnson
ni kujiondoa kwenye foleni, asingeweza kuondoka na kumwacha katika hali hiyo,
akamkumbatia kwa mkono wake wa kuume kisha kumtaka afumbe macho yake ili
wamwombe Mungu pamoja.
“…Mungu mwema, ubaki na mke wangu
mpaka tutakapokutana naye tena, unajua ni kiasi gani nampenda na ningetaka
kubaki hapa Kinshasa pamoja naye, lakini haiwezekani sababu ya majukumu
yaliyoko nyumbani, hivyo basi namwacha mikononi mwako, nasi tubariki katika
safari yetu mpaka tufike Dar es Salaam…” Johnson alimaliza sala yake na kumpiga
busu Loveness usoni kwake.
Kilichofuata baada ya hapo ni
kuingia uwanjani ambako walikaguliwa mizigo yao pamoja na wao wenyewe, kabla
hawajaingia ndani kabisa Johnson akiwa amembeba Melania, aliangalia nje na
kumwona Loveness amesimama palepale walipomwacha, mwanamke mmoja akionekana
kumbembeleza aache kulia.
“Mama bye!” Melania aliongea kwa
sauti ya juu mpaka watu wengine wakageuka.
“I love you Melania!”
“I love you to mom!”
“Take care of yourself and listen to teacher Joyce in the class, okay?” (Ujichunge na msikilize mwalimu Joyce darasani, sawa?)
“Yes mom, I will.” (Ndiyo mama, nitafanya hivyo!)
“Bye baby!” (Kwaheri mpenzi!)
“Bye husband!” (Kwaheri mume wangu!)
“I love you Melania!”
“I love you to mom!”
“Take care of yourself and listen to teacher Joyce in the class, okay?” (Ujichunge na msikilize mwalimu Joyce darasani, sawa?)
“Yes mom, I will.” (Ndiyo mama, nitafanya hivyo!)
“Bye baby!” (Kwaheri mpenzi!)
“Bye husband!” (Kwaheri mume wangu!)
Johnson na mtoto wake wakazama ndani
ya uwanja ambako walikuta pilikapilika za watu wakikimbia huku na kule kujaribu
kuwahi ndege zao, moyoni mwake Johnson alisumbuliwa sana na alichokionyesha mke
wake uwanjani, yeye mwenyewe akaanza kuingiwa na aina fulani ya hofu lakini
akamwamini Mungu na kutembea moja kwa moja hadi chumba cha kusubiria ambako
walikuta tayari abiria wa ndege yao wamekwishaanza kupanda.
Loveness hakuondoka uwanja wa ndege,
alichokifanya ni kusogea nyuma kidogo kuliacha jengo la uwanja katika sehemu
ambayo angeweza kuziona vizuri ndege zilizoruka. Dakika ishirini na tano
baadaye aliiona ndege ndogo ya Shirika la Ndege la Kongo, yenye uwezo wa kubeba
abiria hamsini ikiruka, hiyo ndiyo Johnson na Melania walipanda, akanyanyua
mikono yake juu na kumwomba Mungu aepushe kile ambacho moyo wake ulikuwa
ukikihisia.
***
Ndege ilishaacha sehemu ya mawingu, Johnson na mwanaye Melania walikuwa wameketi vizuri kwenye viti, mkononi Melania alikuwa akichezea michezo ya kompyuta kwenye IPad. Tayari walishatangaziwa kwamba ishara za mikanda zilishaondolewa, hivyo waketi vizuri kwenye viti vyao na kufurahia safari.
***
Ndege ilishaacha sehemu ya mawingu, Johnson na mwanaye Melania walikuwa wameketi vizuri kwenye viti, mkononi Melania alikuwa akichezea michezo ya kompyuta kwenye IPad. Tayari walishatangaziwa kwamba ishara za mikanda zilishaondolewa, hivyo waketi vizuri kwenye viti vyao na kufurahia safari.
Walikuwa wakipita kwenye futi
ishirini na tano elfu juu ya usawa wa bahari, hali ya hewa ilikuwa safi kabisa,
ndege imetulia kama vile walikuwa sebuleni nyumbani kwao. Wahudumu wa ndege
waliwafikia na kuwauliza kile walichohitaji kutumia, Johnson akaagiza chai na
kwa ajili ya mtoto wake akaagiza juisi ya sharubati pamoja na pakiti ya
korosho.
Juisi zilipowekwa tu juu ya meza,
ghafla mlipuko mkubwa sana ukatokea na harufu ya kama kitu kilikuwa kinaungua
ikasikika! Abiria wote ndani ya ndege wakapatwa na mshtuko na kelele zikaanza
kusikika, ingawa wafanyakazi ndani ya ndege hiyo walijitahidi kama hapakuwa na
kitu kilichotokea kwa kuweka tabasamu usoni, abiria walishagundua kwamba tatizo
kubwa lilikuwa limetokea.
Troli lililobeba chakula na vinywaji
likaanza kusukumwa kuondolewa katikati mpaka sehemu yake, wahudumu wakaketi
kwenye viti na kufunga mikanda, abiria wote wakatakiwa kufanya hivyo. Sekunde
chache baadaye sauti ya rubani ikasikika akiwaeleza kwamba injini moja ya ndege
yao ilikuwa imelipuka na kusimama kufanya kazi, hivyo walikuwa wanatumia injini
moja tu, akawatuliza kwa kuwaambia wasiwe na wasiwasi kwani kwa injini moja
wangeweza kufika angalau Bujumbura ambako wangetua kwa dharura.
Watu wakatulia kidogo baada ya
kuelezwa maneno hayo, haikuwa hivyo kwa Melania ambaye alikuwa akilia kwa nguvu
huku akitaja jina la mama yake. Kazi ya Johnson ikawa ni kumtuliza na kumwambia
kila kitu kingekuwa sawa, ingawa kichwani mwake akielewa kabisa walikuwa katika
hatari na kwamba kumbe Loveness alikuwa ameona kitu kilichokuwa kinakwenda
kutokea.
Hali ilikuwa mbaya, ndege sasa
ilikuwa ikienda kwa mwendo wa taratibu kuliko mwanzo huku harufu ya kitu
kilichokuwa kinaungua ikisikika na moshi ukiingia ndani ya ndege kiasi cha watu
kuanza kukohoa. Melania alikohoa sana pengine kuliko watu wengine, Johnson
akachanganyikiwa kabisa.
Vifaa vya kupumulia vikashuka kutoka eneo la juu la kuhifadhia mizigo, Johnson akachukua kimoja na kumvisha mtoto wake kisha yeye mwenyewe kuvaa cha kwake, vikasaidia kidogo katika upumuaji. Ghafla ndege ikaanza kuyumba kuliko ilivyokuwa hapo awali.
Vifaa vya kupumulia vikashuka kutoka eneo la juu la kuhifadhia mizigo, Johnson akachukua kimoja na kumvisha mtoto wake kisha yeye mwenyewe kuvaa cha kwake, vikasaidia kidogo katika upumuaji. Ghafla ndege ikaanza kuyumba kuliko ilivyokuwa hapo awali.
Dakika kama kumi hivi baadaye
mlipuko mwingine wa pili ulisikika tena, moshi ukazidi ndani na ndege badala ya
kwenda mbele ikaanza kushuka kwenda chini! Sauti iliyosikika kupitia kwenye
kipaza sauti ilikuwa ni ya rubani akiwatangazia abiria kwamba injini zote za
ndege zilikuwa zimelipuka na sasa ndege yao ilikuwa ikienda chini kwa kasi
ambako ingejipiga chini.
“Kila mmoja wetu anaweza kusali kwa dini yake, pengine Mungu anaweza kutunusuru!” ilikuwa ni sauti ya rubani.
“Kila mmoja wetu anaweza kusali kwa dini yake, pengine Mungu anaweza kutunusuru!” ilikuwa ni sauti ya rubani.
Hapo ndipo Johnson akaelewa kwamba
kweli walikuwa wanakufa, akamsogeza mtoto wake karibu na kuanza kulia huku
akimwomba Mungu atende muujiza wowote ambao angeweza, taswira ya Loveness
akilia uwanja wa ndege iliendelea kumwijia, akajuta ni kwa nini hakumsikiliza.
“Dad are we going to die!”(Baba, tunakufa?)
“No! We can’t die, just pray!”(Hapana, hatuwezi kufa, sali tu!) Johnson alimwambia Melania ingawa alikuwa na uhakika kabisa kilichosemwa na mtoto wake kilikuwa kweli.
Ndege ilikuwa ikishuka kwa kasi mno kiasi cha kuhisi utumbo ulitaka kupitia mdomoni, Melania alikuwa akilia kwa nguvu na kuita jina la mama yake.
***
Nisingependa kumaliza hadithi hii ya leo bila kukumbusha jambo muhimu la kutoa maisha yako kwa Mungu. Maisha tuliyonayo hapa duniani ni mafupi sana, yanapita kama maua yachanuavyo na kunyauka. Wengi unaowafahamu wamekufa lakini wewe unapumua, ni vyema basi kufikiria maisha baada ya kifo.
Kila siku jiulize: “Hivi nikifa leo nitakwenda jehanam au peponi?” Kila mmoja wetu analo jibu lake, bila shaka sote tungependa kwenda peponi. Kama hivyo ndivyo, basi tiketi ya kwenda huko ni matendo mema na kujiepusha na uovu.
Tukumbuke mshahara wa dhambi ni mauti, bali karama ya Mungu ni uzima wa milele.
Je, nini kitaendelea katika hadithi hii ya kusikitisha? Watakufa?.
“Dad are we going to die!”(Baba, tunakufa?)
“No! We can’t die, just pray!”(Hapana, hatuwezi kufa, sali tu!) Johnson alimwambia Melania ingawa alikuwa na uhakika kabisa kilichosemwa na mtoto wake kilikuwa kweli.
Ndege ilikuwa ikishuka kwa kasi mno kiasi cha kuhisi utumbo ulitaka kupitia mdomoni, Melania alikuwa akilia kwa nguvu na kuita jina la mama yake.
***
Nisingependa kumaliza hadithi hii ya leo bila kukumbusha jambo muhimu la kutoa maisha yako kwa Mungu. Maisha tuliyonayo hapa duniani ni mafupi sana, yanapita kama maua yachanuavyo na kunyauka. Wengi unaowafahamu wamekufa lakini wewe unapumua, ni vyema basi kufikiria maisha baada ya kifo.
Kila siku jiulize: “Hivi nikifa leo nitakwenda jehanam au peponi?” Kila mmoja wetu analo jibu lake, bila shaka sote tungependa kwenda peponi. Kama hivyo ndivyo, basi tiketi ya kwenda huko ni matendo mema na kujiepusha na uovu.
Tukumbuke mshahara wa dhambi ni mauti, bali karama ya Mungu ni uzima wa milele.
Je, nini kitaendelea katika hadithi hii ya kusikitisha? Watakufa?.
Nice story
ReplyDeleteAsante Mkuu japo umenifanya nilie
ReplyDeleteNimelia
ReplyDeletesehemu ya pili pls
ReplyDeleteGud
ReplyDeleteSehemu ya pili
Delete😭😭😭 hadi huruma
ReplyDelete