Monday 7 April 2014

NAKUTANA NA MASHABIKI WENYE MAPENZI YA KILA AINA ,ILA HUYU ALIYEANGUA KILIO AKIOMBA TUONANE NA KUPIGA PICHA KATISHA




 Usiku uliopita umekuwa ni usiku wa furaha kwangu,baada
 ya dada angu kuzindua video yake ya WANATETEMEKA
 kwa,mafanikio makubwa..lakin tukio la huyu kijana 
aliyeangua kilio  akishinikiza anione
 na kupiga picha,ni tukio ambalo limenionesha ni kiasi gani nina
 watu out there walio upande wangu,watu
 wanaonipenda kwa dhat kabisa.
nikiwa backstage
 kulikokuwa kumejaa kidogo,alijitokeza kijana huyu
ambaye
bahat mbaya sikuweza kumwona mapema..
mpaka niliposkia akilia,alikuwa akishinikiza
 apewe nafasi ya kuniona na kupiga picha,but kulingana
 na utaratibu wa kiusalama mlinzi alimzuia na ndipo 
alipoanza kulia mfululizo..na hata alipopata 
nafasi tukaonana na kupiga picha ni kama nilimwongeza spiidi ya kuendelea kulia
 mpka mda wangu wa kupanda stejini ulipofika..
nilipomaliza show na kurudi garini tayari kwa
 kuondoka alinifata akiwa na ombi lile lile,kupiga
 picha nilishuka nikazungumza nae kisha tukapiga picha na kuagana ....!!
NAWAPENDA SANA MASHABIKI WANGU
 Backstage.furaha iliporudi, baada ya kuonana nae na kupiga picha wote
 Hakuishia kule,hata nilipomaliza show alinifata
 kwenye gari tena..mda huu nilikuwa nikifabya mahojiano na Clouds TV
 Nikijaribu kumbembeleza 
 Nikimpa mkono,lakini hii haikuwa shida yake,alitaka tupige picha tena 

Ilinibidi nishuke kabisa kwenye gari ,nikazungumza
 nae na tukapiga picha ndipo akatulia

Akielezdea furaha yake na sababu ya kufanya vile

No comments:

Post a Comment